Mt. 25:6-11 Swahili Union Version (SUV)

6. Lakini usiku wa manane, pakawa na kelele, Haya, bwana arusi; tokeni mwende kumlaki.

7. Mara wakaondoka wanawali wale wote, wakazitengeneza taa zao.

8. Wale wapumbavu wakawaambia wenye busara, Tupeni mafuta yenu kidogo; maana taa zetu zinazimika.

9. Lakini wale wenye busara wakawajibu, wakisema, Sivyo; hayatatutosha sisi na ninyi; afadhali shikeni njia mwende kwa wauzao, mkajinunulie.

10. Na hao walipokuwa wakienda kununua, bwana arusi akaja, nao waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye arusini; mlango ukafungwa.

11. Halafu wakaja na wale wanawali wengine, wakasema, Bwana, Bwana, utufungulie.

Mt. 25