7. Kwa maana taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme; kutakuwa na njaa, na matetemeko ya nchi mahali mahali.
8. Hayo yote ndiyo mwanzo wa utungu.
9. Wakati huo watawasaliti ninyi mpate dhiki, nao watawaua; nanyi mtakuwa watu wa kuchukiwa na mataifa yote kwa ajili ya jina langu.
10. Ndipo wengi watakapojikwaa, nao watasalitiana, na kuchukiana.
11. Na manabii wengi wa uongo watatokea, na kudanganya wengi.
12. Na kwa sababu ya kuongezeka maasi, upendo wa wengi utapoa.
13. Lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka.
14. Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja.
15. Basi hapo mtakapoliona chukizo la uharibifu, lile lililonenwa na nabii Danieli, limesimama katika patakatifu (asomaye na afahamu),
16. ndipo walio katika Uyahudi na wakimbilie milimani;