Mt. 24:46-51 Swahili Union Version (SUV)

46. Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta akifanya hivyo.

47. Amin, nawaambieni, atamweka juu ya vitu vyake vyote.

48. Lakini mtumwa yule mbaya akisema moyoni mwake, Bwana wangu anakawia;

49. akaanza kuwapiga wajoli wake, na kula na kunywa pamoja na walevi;

50. bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani, na saa asiyojua,

51. atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wanafiki; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.

Mt. 24