Mt. 24:45-51 Swahili Union Version (SUV)

45. Ni nani basi yule mtumwa mwaminifu mwenye akili, ambaye bwana wake alimweka juu ya nyumba yake, awape watu chakula kwa wakati wake?

46. Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta akifanya hivyo.

47. Amin, nawaambieni, atamweka juu ya vitu vyake vyote.

48. Lakini mtumwa yule mbaya akisema moyoni mwake, Bwana wangu anakawia;

49. akaanza kuwapiga wajoli wake, na kula na kunywa pamoja na walevi;

50. bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani, na saa asiyojua,

51. atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wanafiki; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.

Mt. 24