Mt. 24:25-29 Swahili Union Version (SUV)

25. Tazama, nimekwisha kuwaonya mbele.

26. Basi wakiwaambia, Yuko jangwani, msitoke; yumo nyumbani, msisadiki.

27. Kwa maana kama vile umeme utokavyo mashariki ukaonekana hata magharibi, hivyo ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.

28. Kwa kuwa po pote ulipo mzoga, ndipo watakapokusanyika tai.

29. Lakini mara, baada ya dhiki ya siku zile, jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwanga wake, na nyota zitaanguka mbinguni, na nguvu za mbinguni zitatikisika;

Mt. 24