16. ndipo walio katika Uyahudi na wakimbilie milimani;
17. naye aliye juu ya dari asishuke kuvichukua vitu vilivyomo nyumbani mwake;
18. wala aliye shambani asirudi nyuma kuichukua nguo yake.
19. Ole wao wenye mimba na wanyonyeshao siku hizo!
20. Ombeni, ili kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi, wala siku ya sabato.
21. Kwa kuwa wakati huo kutakuwapo dhiki kubwa, ambayo haijatokea namna yake tangu mwanzo wa ulimwengu hata sasa, wala haitakuwapo kamwe.
22. Na kama siku hizo zisingalifupizwa, asingeokoka mtu ye yote; lakini kwa ajili ya wateule zitafupizwa siku hizo.
23. Wakati huo mtu akiwaambia, Tazama, Kristo yupo hapa, au yuko kule msisadiki.
24. Kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, kama yamkini, hata walio wateule.
25. Tazama, nimekwisha kuwaonya mbele.
26. Basi wakiwaambia, Yuko jangwani, msitoke; yumo nyumbani, msisadiki.
27. Kwa maana kama vile umeme utokavyo mashariki ukaonekana hata magharibi, hivyo ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.
28. Kwa kuwa po pote ulipo mzoga, ndipo watakapokusanyika tai.
29. Lakini mara, baada ya dhiki ya siku zile, jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwanga wake, na nyota zitaanguka mbinguni, na nguvu za mbinguni zitatikisika;