Mt. 23:6-13 Swahili Union Version (SUV)

6. hupenda viti vya mbele katika karamu, na kuketi mbele katika masinagogi,

7. na kusalimiwa masokoni, na kuitwa na watu, Rabi.

8. Bali ninyi msiitwe Rabi, maana mwalimu wenu ni mmoja, nanyi nyote ni ndugu.

9. Wala msimwite mtu baba duniani; maana Baba yenu ni mmoja, aliye wa mbinguni.

10. Wala msiitwe viongozi; maana kiongozi wenu ni mmoja, naye ndiye Kristo.

11. Naye aliye mkubwa wenu atakuwa mtumishi wenu.

12. Na ye yote atakayejikweza, atadhiliwa; na ye yote atakayejidhili, atakwezwa.

13. Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnawafungia watu ufalme wa mbinguni; ninyi wenyewe hamwingii, wala wanaoingia hamwaachi waingie.

Mt. 23