Mt. 23:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Kisha Yesu akawaambia makutano na wanafunzi wake, akasema,

2. Waandishi na Mafarisayo wameketi katika kiti cha Musa;

3. basi, yo yote watakayowaambia, myashike na kuyatenda; lakini kwa mfano wa matendo yao, msitende; maana wao hunena lakini hawatendi.

4. Wao hufunga mizigo mizito na kuwatwika watu mabegani mwao; wasitake wenyewe kuigusa kwa kidole chao.

5. Tena matendo yao yote huyatenda ili kutazamwa na watu; kwa kuwa hupanua hirizi zao, huongeza matamvua yao;

Mt. 23