Mt. 22:3-7 Swahili Union Version (SUV)

3. Akawatuma watumwa wake wawaite walioalikwa kuja arusini; nao wakakataa kuja.

4. Akatuma tena watu kwa wengine, akisema, Waambieni wale walioalikwa, Tazameni, nimeandaa karamu yangu; ng’ombe zangu na vinono vimekwisha kuchinjwa, na vyote vimekuwa tayari, njoni arusini.

5. Lakini hawakujali, wakaenda zao, mmoja shambani kwake, mmoja kwenye biashara yake;

6. nao waliosalia wakawakamata watumwa wake, wakawatenda jeuri, na kuwaua.

7. Basi yule mfalme akaghadhibika; akapeleka majeshi yake, akawaangamiza wauaji wale, akauteketeza mji wao.

Mt. 22