Mt. 22:1-9 Swahili Union Version (SUV)

1. Yesu akajibu, akawaambia tena kwa mithali, akisema,

2. Ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyemfanyia mwanawe arusi.

3. Akawatuma watumwa wake wawaite walioalikwa kuja arusini; nao wakakataa kuja.

4. Akatuma tena watu kwa wengine, akisema, Waambieni wale walioalikwa, Tazameni, nimeandaa karamu yangu; ng’ombe zangu na vinono vimekwisha kuchinjwa, na vyote vimekuwa tayari, njoni arusini.

5. Lakini hawakujali, wakaenda zao, mmoja shambani kwake, mmoja kwenye biashara yake;

6. nao waliosalia wakawakamata watumwa wake, wakawatenda jeuri, na kuwaua.

7. Basi yule mfalme akaghadhibika; akapeleka majeshi yake, akawaangamiza wauaji wale, akauteketeza mji wao.

8. Kisha akawaambia watumwa wake, Arusi i tayari, lakini wale walioalikwa hawakustahili.

9. Basi enendeni hata njia panda za barabara, na wote mwaonao waiteni arusini.

Mt. 22