Mt. 22:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Yesu akajibu, akawaambia tena kwa mithali, akisema,

2. Ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyemfanyia mwanawe arusi.

3. Akawatuma watumwa wake wawaite walioalikwa kuja arusini; nao wakakataa kuja.

4. Akatuma tena watu kwa wengine, akisema, Waambieni wale walioalikwa, Tazameni, nimeandaa karamu yangu; ng’ombe zangu na vinono vimekwisha kuchinjwa, na vyote vimekuwa tayari, njoni arusini.

5. Lakini hawakujali, wakaenda zao, mmoja shambani kwake, mmoja kwenye biashara yake;

Mt. 22