4. Haya yote yamekuwa, ili litimie neno lililonenwa na nabii, akisema,
5. Mwambieni binti SayuniTazama, mfalme wako anakuja kwako,Mpole, naye amepanda punda,Na mwana-punda, mtoto wa punda.
6. Wale wanafunzi wakaenda zao, wakafanya kama Yesu alivyowaamuru,
7. wakamleta yule punda na mwana-punda, wakaweka nguo zao juu yao, naye akaketi juu yake.
8. Watu wengi katika ule mkutano wakatandaza nguo zao njiani; na wengine wakakata matawi ya miti, wakayatandaza njiani.
9. Na makutano waliotangulia, na wale waliofuata, wakapaza sauti, wakisema, Hosana, Mwana wa Daudi; ndiye mbarikiwa, yeye ajaye kwa jina la Bwana; Hosana juu mbinguni.