9. Na walipokuja wale wa saa kumi na moja, walipokea kila mtu dinari.
10. Na wale wa kwanza walipokuja, walidhani kwamba watapokea zaidi; na hao pia wakapokea kila mtu dinari.
11. Basi wakiisha kuipokea, wakamnung’unikia mwenye nyumba,
12. wakisema, Hao wa mwisho wametenda kazi saa moja tu, nawe umewasawazisha na sisi tuliostahimili taabu na hari za mchana kutwa.