1. Kwa maana ufalme wa mbinguni umefanana na mtu mwenye nyumba aliyetoka alfajiri kwenda kuajiri wakulima awapeleke katika shamba lake la mizabibu.
2. Naye alipokwisha kupatana na wakulima kuwapa kutwa dinari, aliwapeleka katika shamba lake la mizabibu.
3. Akatoka mnamo saa tatu, akaona wengine wamesimama sokoni wasiokuwa na kazi;
4. na hao nao akawaambia, Enendeni nanyi katika shamba langu la mizabibu, na iliyo haki nitawapa. Wakaenda.
5. Akatoka tena mnamo saa sita na saa kenda, akafanya vile vile.