21. Kisha Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara saba?
22. Yesu akamwambia, Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.
23. Kwa sababu hii ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake.
24. Alipoanza kuifanya, aliletewa mtu mmoja awiwaye talanta elfu kumi.