Mt. 17:1-7 Swahili Union Version (SUV)

1. Na baada ya siku sita Yesu akawatwaa Petro, na Yakobo, na Yohana nduguye, akawaleta juu ya mlima mrefu faraghani;

2. akageuka sura yake mbele yao; uso wake ukang’aa kama jua, mavazi yake yakawa meupe kama nuru.

3. Na tazama, wakatokewa na Musa na Eliya, wakizungumza naye.

4. Petro akajibu akamwambia Yesu, Bwana, ni vizuri sisi kuwapo hapa; ukitaka, nitafanya hapa vibanda vitatu, kimoja chako wewe, na kimoja cha Musa, na kimoja cha Eliya.

5. Alipokuwa katika kusema, tazama, wingu jeupe likawatia uvuli; na tazama, sauti ikatoka katika lile wingu, ikasema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye; msikieni yeye.

6. Na wale wanafunzi waliposikia, walianguka kifulifuli, wakaogopa sana.

7. Yesu akaja, akawagusa, akasema, Inukeni, wala msiogope.

Mt. 17