Mt. 15:33-39 Swahili Union Version (SUV)

33. Wanafunzi wake wakamwambia, Tupate wapi mikate mingi hapa nyikani, hata kushibisha mkutano mkuu namna hii?

34. Yesu akawaambia, Mnayo mikate mingapi? Wakasema, Saba, na visamaki vichache.

35. Akawaagiza mkutano waketi chini;

36. akaitwaa ile mikate saba na vile visamaki, akashukuru akavimega, akawapa wanafunzi wake, nao wanafunzi wakawapa makutano.

37. Wakala wote wakashiba; wakayaokota masazo ya vipande vya mikate makanda saba, yamejaa.

38. Nao waliokula walikuwa wanaume elfu nne, bila wanawake na watoto.

39. Akawaaga makutano, akapanda chomboni, akaenda pande za Magadani.

Mt. 15