33. Wanafunzi wake wakamwambia, Tupate wapi mikate mingi hapa nyikani, hata kushibisha mkutano mkuu namna hii?
34. Yesu akawaambia, Mnayo mikate mingapi? Wakasema, Saba, na visamaki vichache.
35. Akawaagiza mkutano waketi chini;
36. akaitwaa ile mikate saba na vile visamaki, akashukuru akavimega, akawapa wanafunzi wake, nao wanafunzi wakawapa makutano.