3. Maana Herode alikuwa amemkamata Yohana, akamfunga, akamtia gerezani, kwa ajili ya Herodia, mke wa Filipo nduguye.
4. Kwa sababu Yohana alimwambia, Si halali kwako kuwa naye.
5. Naye alipotaka kumwua, aliwaogopa watu, maana walimwona Yohana kuwa nabii.
6. Hata ilipofika sikukuu ya kuzaliwa kwake Herode, binti Herodia alicheza mbele ya watu, akampendeza Herode.