1. Wakati ule mfalme Herode alisikia habari za Yesu, akawaambia watumishi wake,
2. Huyo ndiye Yohana Mbatizaji; amefufuka katika wafu; na kwa hiyo nguvu hizo zinatenda kazi ndani yake.
3. Maana Herode alikuwa amemkamata Yohana, akamfunga, akamtia gerezani, kwa ajili ya Herodia, mke wa Filipo nduguye.
4. Kwa sababu Yohana alimwambia, Si halali kwako kuwa naye.
5. Naye alipotaka kumwua, aliwaogopa watu, maana walimwona Yohana kuwa nabii.