Mt. 12:14-21 Swahili Union Version (SUV)

14. Lakini wale Mafarisayo wakatoka wakafanya shauri juu yake jinsi ya kumwangamiza.

15. Naye Yesu hali akiyafahamu hayo akaondoka huko; na watu wengi wakamfuata; akawaponya wote,

16. akawakataza wasimdhihirishe;

17. ili litimie neno lililonenwa na nabii Isaya, akisema,

18. Tazama, mtumishi wangu niliyemteua;Mpendwa wangu, moyo wangu uliyependezwa naye;Nitatia roho yangu juu yake,Naye atawatangazia Mataifa hukumu.

19. Hatateta wala hatapaza sauti yake;Wala mtu hatasikia sauti yake njiani.

20. Mwanzi uliopondeka hatauvunja,Wala utambi utokao moshi hatauzima,Hata ailetapo hukumu ikashinda.

21. Na jina lake Mataifa watalitumainia.

Mt. 12