Mt. 11:28-30 Swahili Union Version (SUV)

28. Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30. kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.

Mt. 11