7. Nao waniabudu bure,Wakifundisha mafundishoYaliyo maagizo ya wanadamu,
8. Ninyi mwaiacha amri ya Mungu, na kuyashika mapokeo ya wanadamu.
9. Akawaambia, Vema! Mwaikataa amri ya Mungu mpate kuyashika mapokeo yenu.
10. Maana Musa alisema, Waheshimu baba yako na mama yako, na, Amtukanaye babaye au mamaye kufa na afe.
11. Bali ninyi husema, Mtu akimwambia babaye au mamaye, Ni Korbani, yaani, wakfu, kitu changu cho chote kikupasacho kufaidiwa nacho, huwa basi;
12. wala hammruhusu baada ya hayo kumtendea neno babaye au mamaye;