Mk. 7:5-10 Swahili Union Version (SUV)

5. Basi wale Mafarisayo na waandishi wakamwuliza, Mbona wanafunzi wako hawaendi kwa kuyafuata mapokeo ya wazee, bali hula chakula kwa mikono najisi?

6. Akawaambia, Isaya alitabiri vema juu yenu ninyi wanafiki, kama ilivyoandikwa,Watu hawa huniheshimu kwa midomoIla mioyo yao iko mbali nami;

7. Nao waniabudu bure,Wakifundisha mafundishoYaliyo maagizo ya wanadamu,

8. Ninyi mwaiacha amri ya Mungu, na kuyashika mapokeo ya wanadamu.

9. Akawaambia, Vema! Mwaikataa amri ya Mungu mpate kuyashika mapokeo yenu.

10. Maana Musa alisema, Waheshimu baba yako na mama yako, na, Amtukanaye babaye au mamaye kufa na afe.

Mk. 7