Mk. 7:34-37 Swahili Union Version (SUV)

34. akatazama juu mbinguni, akaugua, akamwambia, Efatha, maana yake, Funguka.

35. Mara masikio yake yakafunguka, kifungo cha ulimi wake kikalegea, akasema vizuri.

36. Akawaonya wasimwambie mtu; lakini kadiri ya alivyozidi kuwaagiza, ndivyo walivyozidi kutangaza habari;

37. wakashangaa mno kupita kiasi, wakinena, Ametenda mambo yote vema; viziwi awafanya wasikie, na bubu waseme.

Mk. 7