6. Na alipomwona Yesu kwa mbali, alipiga mbio, akamsujudia;
7. akapiga kelele kwa sauti kuu, akasema, Nina nini nawe, Yesu, Mwana wa Mungu aliye juu? Nakuapisha kwa Mungu usinitese.
8. Kwa sababu amemwambia, Ewe pepo mchafu, mtoke mtu huyu.
9. Akamwuliza, Jina lako nani? Akamjibu, Jina langu ni Legioni, kwa kuwa tu wengi.
10. Akamsihi sana asiwapeleke nje ya nchi ile.