22. Akaja mtu mmoja katika wakuu wa sinagogi, jina lake Yairo; hata alipomwona, akaanguka miguuni pake,
23. akimsihi sana, akisema, Binti yangu mdogo yu katika kufa; nakuomba uje, uweke mkono wako juu yake, apate kupona, na kuishi.
24. Akaenda pamoja naye; mkutano mkuu wakamfuata, wakimsonga-songa.
25. Na mwanamke mmoja mwenye kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili,