Mk. 5:21-29 Swahili Union Version (SUV)

21. Hata Yesu alipokwisha kuvuka kurudia ng’ambo katika kile chombo, wakamkusanyikia mkutano mkuu; naye alikuwa kando ya bahari.

22. Akaja mtu mmoja katika wakuu wa sinagogi, jina lake Yairo; hata alipomwona, akaanguka miguuni pake,

23. akimsihi sana, akisema, Binti yangu mdogo yu katika kufa; nakuomba uje, uweke mkono wako juu yake, apate kupona, na kuishi.

24. Akaenda pamoja naye; mkutano mkuu wakamfuata, wakimsonga-songa.

25. Na mwanamke mmoja mwenye kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili,

26. na kuteswa mengi kwa mikono ya matabibu wengi, amegharimiwa vitu vyote alivyo navyo, kusimfae hata kidogo, bali hali yake ilizidi kuwa mbaya

27. aliposikia habari za Yesu, alipita katika mkutano kwa nyuma, akaligusa vazi lake;

28. maana alisema, Nikiyagusa mavazi yake tu, nitapona.

29. Mara chemchemi ya damu yake ikakauka, naye akafahamu mwilini mwake kwamba amepona msiba ule.

Mk. 5