6. hata jua lilipozuka iliungua, na kwa kuwa haina mizizi ikanyauka.
7. Nyingine ikaanguka penye miiba; ile miiba ikamea ikaisonga, isizae matunda.
8. Nyingine zikaanguka penye udongo ulio mzuri, zikazaa matunda, zikimea na kukua, na kuzaa, moja thelathini, moja sitini, na moja mia.
9. Akasema, Aliye na masikio ya kusikilia, na asikie.
10. Naye alipokuwa peke yake, wale watu waliomzunguka, na wale Thenashara, walimwuliza habari za ile mifano.
11. Akawaambia, Ninyi mmejaliwa kuijua siri ya ufalme wa Mungu, bali kwa wale walio nje yote hufanywa kwa mifano,
12. ili wakitazama watazame, wasione;Na wakisikia wasikie, wasielewe;Wasije wakaongoka, na kusamehewa.
13. Akawaambia, Hamjui mfano huu? Basi mifano yote mtaitambuaje?
14. Mpanzi huyo hulipanda neno.
15. Hawa ndio walio kando ya njia lipandwapo neno; nao, wakiisha kusikia, mara huja Shetani, akaliondoa lile neno lililopandwa mioyoni mwao.
16. Kadhalika na hawa ndio wapandwao penye miamba, ambao kwamba wakiisha kulisikia lile neno, mara hulipokea kwa furaha;