25. Kwa maana mwenye kitu atapewa, naye asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyang’anywa.
26. Akasema, Ufalme wa Mungu, mfano wake ni kama mtu aliyemwaga mbegu juu ya nchi;
27. akawa akilala na kuondoka, usiku na mchana, nayo mbegu ikamea na kukua, asivyojua yeye.
28. Maana nchi huzaa yenyewe; kwanza jani, tena suke, kisha ngano pevu katika suke.
29. Hata matunda yakiiva, mara atapeleka mundu, kwa kuwa mavuno yamefika.