Mk. 4:12-16 Swahili Union Version (SUV)

12. ili wakitazama watazame, wasione;Na wakisikia wasikie, wasielewe;Wasije wakaongoka, na kusamehewa.

13. Akawaambia, Hamjui mfano huu? Basi mifano yote mtaitambuaje?

14. Mpanzi huyo hulipanda neno.

15. Hawa ndio walio kando ya njia lipandwapo neno; nao, wakiisha kusikia, mara huja Shetani, akaliondoa lile neno lililopandwa mioyoni mwao.

16. Kadhalika na hawa ndio wapandwao penye miamba, ambao kwamba wakiisha kulisikia lile neno, mara hulipokea kwa furaha;

Mk. 4