Mk. 3:20-25 Swahili Union Version (SUV)

20. Mkutano wakakusanyika tena, hata wao wenyewe wasiweze hata kula mkate.

21. Jamaa zake walipopata habari wakatoka kwenda kumkamata; maana walisema, Amerukwa na akili.

22. Nao waandishi walioshuka kutoka Yerusalemu wakasema, Ana Beelzebuli, na, Kwa mkuu wa pepo huwatoa pepo.

23. Akawaita, akawaambia kwa mifano, Awezaje Shetani kumtoa Shetani?

24. Na ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, ufalme huo hauwezi kusimama;

25. na nyumba ikifitinika juu ya nafsi yake, nyumba hiyo haiwezi kusimama.

Mk. 3