11. Na pepo wachafu, kila walipomwona, walianguka mbele yake, wakalia wakisema, Wewe ndiwe Mwana wa Mungu.
12. Akawakataza sana, wasimdhihirishe.
13. Akapanda mlimani, akawaita aliowataka mwenyewe; wakamwendea.
14. Akaweka watu kumi na wawili, wapate kuwa pamoja naye, na kwamba awatume kuhubiri,
15. tena wawe na amri ya kutoa pepo.
16. Akawaweka wale Thenashara; na Simoni akampa jina la Petro;