Mk. 3:11-16 Swahili Union Version (SUV)

11. Na pepo wachafu, kila walipomwona, walianguka mbele yake, wakalia wakisema, Wewe ndiwe Mwana wa Mungu.

12. Akawakataza sana, wasimdhihirishe.

13. Akapanda mlimani, akawaita aliowataka mwenyewe; wakamwendea.

14. Akaweka watu kumi na wawili, wapate kuwa pamoja naye, na kwamba awatume kuhubiri,

15. tena wawe na amri ya kutoa pepo.

16. Akawaweka wale Thenashara; na Simoni akampa jina la Petro;

Mk. 3