10. Maana aliponya wengi, hata wote waliokuwa na misiba wakamrukia wapate kumgusa.
11. Na pepo wachafu, kila walipomwona, walianguka mbele yake, wakalia wakisema, Wewe ndiwe Mwana wa Mungu.
12. Akawakataza sana, wasimdhihirishe.
13. Akapanda mlimani, akawaita aliowataka mwenyewe; wakamwendea.
14. Akaweka watu kumi na wawili, wapate kuwa pamoja naye, na kwamba awatume kuhubiri,
15. tena wawe na amri ya kutoa pepo.
16. Akawaweka wale Thenashara; na Simoni akampa jina la Petro;
17. na Yakobo, mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye Yakobo, akawapa jina la Boanerge, maana yake, wana wa ngurumo;
18. na Andrea, na Filipo, na Bartholomayo, na Mathayo, na Tomaso, na Yakobo wa Alfayo, na Thadayo, na Simoni Mkananayo,
19. na Yuda Iskariote, ndiye aliyemsaliti.Kisha akaingia nyumbani.
20. Mkutano wakakusanyika tena, hata wao wenyewe wasiweze hata kula mkate.
21. Jamaa zake walipopata habari wakatoka kwenda kumkamata; maana walisema, Amerukwa na akili.
22. Nao waandishi walioshuka kutoka Yerusalemu wakasema, Ana Beelzebuli, na, Kwa mkuu wa pepo huwatoa pepo.
23. Akawaita, akawaambia kwa mifano, Awezaje Shetani kumtoa Shetani?
24. Na ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, ufalme huo hauwezi kusimama;
25. na nyumba ikifitinika juu ya nafsi yake, nyumba hiyo haiwezi kusimama.