Mk. 3:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Akaingia tena katika sinagogi; na palikuwako huko mtu mwenye mkono uliopooza;

2. wakamvizia ili kuona kama atamponya siku ya sabato; wapate kumshitaki.

3. Akamwambia yule mtu mwenye mkono uliopooza, Simama katikati.

4. Akawauliza, Ni halali siku ya sabato kutenda mema, au kutenda mabaya? Kuponya roho au kuiua? Wakanyamaza.

Mk. 3