3. Hata alipokuwa ameketi katika mlima wa Mizeituni, kuelekea hekalu Petro, na Yakobo, na Yohana, na Andrea walimwuliza kwa faragha,
4. Tuambie, mambo hayo yatakuwa lini? Nayo ni nini dalili ya wakati, hayo yote yatakapokuwa karibu kutimia?
5. Yesu akaanza kuwaambia, Jihadharini, mtu asiwadanganye.
6. Wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, Mimi ndiye, nao watadanganya wengi.