Mk. 13:21-25 Swahili Union Version (SUV)

21. Na wakati huo mtu akiwaambia, Tazama, Kristo yupo hapa, au yuko kule, msisadiki;

22. kwa maana wataondoka Makristo wa uongo, na manabii wa uongo, watatoa ishara na maajabu, wapate kuwadanganya, kama yamkini, hata hao wateule.

23. Bali ninyi jihadharini; nimekwisha kuwaonya yote mbele.

24. Lakini siku zile, baada ya dhiki hiyo, jua litatiwa giza, na mwezi hatautoa mwanga wake.

25. na nyota za mbinguni zitakuwa zikianguka, na nguvu zilizo mbinguni zitatikisika.

Mk. 13