Mk. 12:9-13 Swahili Union Version (SUV)

9. basi atafanyaje yule bwana wa shamba la mizabibu? Atakuja na kuwaangamiza wale wakulima, na lile shamba la mizabibu atawapa wengine.

10. Hata andiko hili hamjalisoma,Jiwe walilolikataa waashi,Hilo limekuwa jiwe kuu la pembeni.

11. Neno hili limetoka kwa Bwana,Nalo ni ajabu machoni petu?

12. Nao wakatafuta kumkamata, wakaogopa mkutano; maana walitambua ya kwamba ule mfano amewanenea wao. Wakamwacha wakaenda zao.

13. Wakatuma kwake baadhi ya Mafarisayo na Maherodi, ili wamnase kwa maneno.

Mk. 12