6. Wakawaambia kama Yesu alivyowaagiza, nao wakawaruhusu.
7. Wakamletea Yesu yule mwana-punda, wakatandika mavazi yao juu yake; akaketi juu yake.
8. Watu wengi wakatandaza mavazi yao njiani, na wengine matawi waliyoyakata mashambani.
9. Nao watu waliotangulia na wale waliofuata wakapaza sauti, Hosana; ndiye mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana;
10. umebarikiwa na ufalme ujao, wa baba yetu Daudi. Hosana juu mbinguni.