Mk. 11:6-10 Swahili Union Version (SUV)

6. Wakawaambia kama Yesu alivyowaagiza, nao wakawaruhusu.

7. Wakamletea Yesu yule mwana-punda, wakatandika mavazi yao juu yake; akaketi juu yake.

8. Watu wengi wakatandaza mavazi yao njiani, na wengine matawi waliyoyakata mashambani.

9. Nao watu waliotangulia na wale waliofuata wakapaza sauti, Hosana; ndiye mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana;

10. umebarikiwa na ufalme ujao, wa baba yetu Daudi. Hosana juu mbinguni.

Mk. 11