Mk. 11:10-14 Swahili Union Version (SUV)

10. umebarikiwa na ufalme ujao, wa baba yetu Daudi. Hosana juu mbinguni.

11. Naye akaingia Yerusalemu hata ndani ya hekalu; na alipokwisha kutazama yote pande zote, kwa kuwa ni wakati wa jioni, akatoka, akaenda Bethania pamoja na wale Thenashara.

12. Hata asubuhi yake walipotoka Bethania aliona njaa.

13. Akaona kwa mbali mtini wenye majani, akaenda ili labda aone kitu juu yake; na alipoufikilia hakuona kitu ila majani; maana si wakati wa tini.

14. Akajibu, akauambia, Tangu leo hata milele mtu asile matunda kwako. Wanafunzi wake wakasikia.

Mk. 11