Mk. 10:5-10 Swahili Union Version (SUV)

5. Yesu akawaambia, Kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu aliwaandikia amri hii.

6. Lakini tangu mwanzo wa kuumbwa ulimwengu, aliwafanya mume na mke.

7. Kwa sababu hiyo mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe;

8. na hao wawili watakuwa mwili mmoja; hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja.

9. Basi alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.

10. Hata nyumbani tena wanafunzi wakamwuliza habari ya neno hilo.

Mk. 10