3. Naye akajibu, akawaambia, Musa aliwaamuru nini?
4. Wakasema, Musa alitoa ruhusa kuandika hati ya talaka na kumwacha.
5. Yesu akawaambia, Kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu aliwaandikia amri hii.
6. Lakini tangu mwanzo wa kuumbwa ulimwengu, aliwafanya mume na mke.
7. Kwa sababu hiyo mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe;
8. na hao wawili watakuwa mwili mmoja; hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja.
9. Basi alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.