Mk. 1:16-21 Swahili Union Version (SUV)

16. Naye alipokuwa akipita kando ya bahari ya Galilaya, akamwona Simoni na Andrea nduguye, wakitupa jarife baharini; kwa maana walikuwa wavuvi.

17. Yesu akawaambia, Njoni mnifuate, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu.

18. Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.

19. Akaendelea mbele kidogo, akamwona Yakobo wa Zebedayo, na Yohana nduguye, nao pia walikuwa chomboni, wakizitengeneza nyavu zao.

20. Mara akawaita, wakamwacha baba yao Zebedayo ndani ya chombo pamoja na watu wa mshahara, wakaenda, wakamfuata.

21. Wakashika njia mpaka Kapernaumu, na mara siku ya sabato akaingia katika sinagogi, akafundisha.

Mk. 1