Mit. 9:8-18 Swahili Union Version (SUV)

8. Usimkaripie mwenye dharau, asije akakuchukia;Mkaripie mwenye hekima, naye atakupenda.

9. Mwelimishe mwenye hekima, naye atazidi kuwa na hekima;Mfundishe mwenye haki, naye atazidi kuwa na elimu;

10. Kumcha BWANA ni mwanzo wa hekima;Na kumjua Mtakatifu ni ufahamu.

11. Maana, kwa msaada wangu siku zako zitazidishwa;Na miaka ya maisha yako itaongezwa.

12. Kama una hekima, una hekima kwa nafsi yako;Na kama una dharau, utaichukua peke yako.

13. Mwanamke mpumbavu hupiga kelele,Ni mjinga, hajui kitu.

14. Hukaa mlangoni pa nyumba yake,Juu ya kiti mahali pa mjini palipoinuka,

15. Apate kuwaita wapitao njiani,Waendao moja kwa moja katika njia zao.

16. Kila aliye mjinga na aingie humu.Tena amwambia mtu aliyepungukiwa na akili,

17. Maji yaliyoibiwa ni matamu,Na mkate ulioliwa kwa siri hupendeza.

18. Lakini huyo hajui ya kuwa wafu wamo humo;Ya kuwa wageni wake wamo chini kuzimuni.

Mit. 9