Mit. 9:5-13 Swahili Union Version (SUV)

5. Njoo ule mkate wangu,Ukanywe divai niliyoichanganya.

6. Enyi wajinga, acheni ujinga, mkaishi,Mkaende katika njia ya ufahamu.

7. Amkemeaye mwenye dharau hujipatia fedheha;Amkaripiaye mtu mbaya hujipatia aibu.

8. Usimkaripie mwenye dharau, asije akakuchukia;Mkaripie mwenye hekima, naye atakupenda.

9. Mwelimishe mwenye hekima, naye atazidi kuwa na hekima;Mfundishe mwenye haki, naye atazidi kuwa na elimu;

10. Kumcha BWANA ni mwanzo wa hekima;Na kumjua Mtakatifu ni ufahamu.

11. Maana, kwa msaada wangu siku zako zitazidishwa;Na miaka ya maisha yako itaongezwa.

12. Kama una hekima, una hekima kwa nafsi yako;Na kama una dharau, utaichukua peke yako.

13. Mwanamke mpumbavu hupiga kelele,Ni mjinga, hajui kitu.

Mit. 9