Mit. 8:5-10 Swahili Union Version (SUV)

5. Enyi wajinga, fahamuni werevu,Nanyi wapumbavu, mpate moyo wa kufahamu.

6. Sikieni, maana nitasema yaliyo mazuri,Na kufumbua midomo yangu kutakuwa maadili.

7. Maana kinywa changu kitasema kweli,Na uovu ni chukizo kwa midomo yangu.

8. Maneno yote ya kinywa changu yana haki;Hapana hata neno lililopotoka au la ukaidi.

9. Yote humwelea yule afahamuye,Yote huelekea mbele yao waliopata maarifa.

10. Pokea mafundisho yangu, wala si fedha,Na maarifa kuliko dhahabu safi.

Mit. 8