25. Kabla milima haijawekwa imara,Kabla ya vilima nalizaliwa.
26. Alipokuwa hajaiumba dunia, wala makondeWala chanzo cha mavumbi ya dunia;
27. Alipozithibitisha mbingu nalikuwako;Alipopiga duara katika uso wa bahari;
28. Alipofanya imara mawingu yaliyo juu;Chemchemi za bahari zilipopata nguvu;
29. Alipoipa bahari mpaka wake,Kwamba maji yake yasiasi amri yake;Alipoiagiza misingi ya nchi;
30. Ndipo nilipokuwa pamoja naye, kama stadi wa kazi;Nikawa furaha yake kila siku;Nikifurahi daima mbele zake;
31. Nikiifurahia dunia inayokaliwa na watu;Na furaha yangu ilikuwa pamoja na wanadamu.
32. Basi, wanangu, nisikilizeni sasa;Maana heri hao wazishikao amri zangu.