2. Juu ya mahali palipoinuka karibu na njia,Penye njia panda, ndipo asimamapo.
3. Karibu na malango, mahali pa kuingia mjini,Mahali pa kuyaingilia malango anapiga kelele.
4. Enyi watu, nawaita ninyi;Na sauti yangu ni kwa wanadamu.
5. Enyi wajinga, fahamuni werevu,Nanyi wapumbavu, mpate moyo wa kufahamu.
6. Sikieni, maana nitasema yaliyo mazuri,Na kufumbua midomo yangu kutakuwa maadili.