9. Wakati wa magharibi, wakati wa jioni,Usiku wa manane, gizani.
10. Na tazama, mwanamke akamkuta,Ana mavazi ya kikahaba, mwerevu wa moyo;
11. Ana kelele, na ukaidi;Miguu yake haikai nyumbani mwake.
12. Mara yu katika njia kuu, mara viwanjani,Naye huotea kwenye pembe za kila njia.
13. Basi akamshika, akambusu,Akamwambia kwa uso usio na haya,
14. Kwangu ziko sadaka za amani;Leo hivi nimeziondoa nadhiri zangu;