Mit. 7:9-13 Swahili Union Version (SUV)

9. Wakati wa magharibi, wakati wa jioni,Usiku wa manane, gizani.

10. Na tazama, mwanamke akamkuta,Ana mavazi ya kikahaba, mwerevu wa moyo;

11. Ana kelele, na ukaidi;Miguu yake haikai nyumbani mwake.

12. Mara yu katika njia kuu, mara viwanjani,Naye huotea kwenye pembe za kila njia.

13. Basi akamshika, akambusu,Akamwambia kwa uso usio na haya,

Mit. 7